Mwl.Godlisten Urio

Mwl.Godlisten Urio

Share

Teaching the word of God and sharing practical insights on parenting for purposeful generation

22/05/2026

Habari za wakati huu tena ,nawasalimu kwa jina la Yesu,ni matumaini yangu sote ni wazima wa afya.

🖊Leo kwa neema ya Mungu nataka tujifunze kidogo kuhusu fedha,tuangalie kutokea hapa

✍️Mafundisho ya Yesu katika eneo la fedha alitufundisha hivi

Mathayo 6:21
[21]kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.
For where your treasure is, there will your heart be also.

✍️Ikiwa hazina(fedha) ilipo ndipo na moyo wa mtu ulipo ,ina maana fedha(hazina) ina nguvu ya kuuvuta moyo(nafsi),na ikiwa kwenye moyo kuna(akili,,hisia,maamuzi,dhamira nia n.k)

Ina maana fedha ya mtu ilipo ndipo ilipo nia,dhamira,maamuzi,hisia,akili na mambo mengine yanayohitaji nafsi,tukiunganisha na mstari huu

1 Timotheo 6:10
[10]Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.

✍️Kumbuka upendo ni hisia kwa hiyo k**a hazina ya mtu ilipo ndipo na moyo wake ulipo inamaana mtu huyo tayari upendo wake upo kwenye fedha(hazina)

Hivyo tunatazamia matokeo ya mtu huyo katika nyanja ya hisia,maamuzi,dhamira,akili na nia yatakuwa shina la mabaya

✍️Kwa ushahidi wa hili angalia viongozi,watu,watumishi wa Mungu mbalimbali ambao mioyo yao imevutwa na pesa jinsi ambavyo wamekuwa shina la mabaya na uharibifu

✍️Jambo lingine ni hili k**a hazina ya mtu ilipo ndipo na moyo wake ulipo ,ina maana fedha inauwezo wa kubeba moyo wa mtoa fedha

Ndio maana sehemu yeyote ambapo ilitangulizwa fedha ikapokelewa ni rahisi sana na ombi au dhamira,nia,maamuzi,matakwa n.k ya mtoa fedha kutekelezwa na yule aliyeipokea

Leo angalia fedha zinazotolewa k**a misaada mbalimbali katika nchi mbalimbali jinsi ambavyo zinakuja na roho za waliotoa fedha hizo

Lakini angalia kwenye familia maamuzi ya mtu mwenye fedha hata k**a yana madhara yatasikilizwa na kutekelezwa kwa sababu ya ile nguvu iliyomo kwenye fedha imebeba maamuzi yake na kuyapeleka kwenye mioyo ya wale ambao wananufaika na fedha anazokuwa anatoa.

Anagalia mabinti na vijana wangapi leo wamejikuta kwenye mahusiano yenye majuto kwa sababu tuu ilitangulia fedha ikateka mioyo yao ikaielekeza hazina/fedha ilipotoka

Daniel alilitambua hili tokea mwanzo ukisoma sura ya kwanza utaona laikini pia angalia hapa

Danieli 5:17
[17]Ndipo Danieli akajibu, akasema mbele ya mfalme; Zawadi zako zishike wewe mwenyewe; na thawabu zako mpe mtu mwingine; walakini nitamsomea mfalme maandiko haya, na kumjulisha tafsiri yake.

✍️🖊Mungu hakukusudia fedha kuwa na nguvu kuzidi moyo wa mtu ila dhambi ndio ilisababisha ndio maana Yesu akatueleza namna ya kufanya ili badala ya moyo kufuata hazina ,hazina ifuate moyo

Marko 3:27
[27]Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.

✍️Fedha ina nguvu kuliko moyo wa mtu mpaka mtu amemruhusu Mungu kuingia ndani na kuulinda moyo ili awe na nguvu ya kuitawala fedha

Tahadhari:
1.Fedha ni nzuri na inatumika kuleta majibu ya mambo yote na ni ulinzi,hivyo tunapaswa kuitafuta ila tuwe na nguvu ya kuitawala kupitia Kristo,sijasema fedha ni jawabu nimesema inatumika kuleta jawabu

Mhubiri 7:12
[12]Kwa maana hekima ni ulinzi, k**a vile fedha ilivyo ulinzi; na ubora wa maarifa ni ya kwamba hekima humhifadhi yeye aliye nayo.

Mhubiri 10:19
[19]Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko,
Na divai huyafurahisha maisha; Na fedha huleta jawabu la mambo yote.

2.Husifurahie tuu kupokea fedha unayopewa jaribu kutafakari na kumuomba Mungu kwa msaada wa Roho Mtakatifu kujua fedha hiyo imebeba roho ipi?

Kuna wengi maisha yao yalibadilika kabisa baada ya kupokea fedha kutoka kwa watu mbalimbali

Mungu akubariki sana asantee kwa kujifunza na mimi ,ukiona vema na kupata neema mshirikishe na mwingine

07/05/2026

Hello habari za wakati huu tena
Karibu kwa pamoja tushiriki mkate huu kwa siku ya leo

Kwa neema ya Mungu leo nataka tuangalie kuhusu familia

Napenda tauanze kutokea hapa

✍️Mungu alipokuwa anamuumba mtu alisema na tumfanye mtu kwa sura na mfano wetu akiwa na maana

✝️Kwa sura kiasili,kitabia,kimwenendo,kitamaduni

✝️Kwa mfano
Kiutendaji kwamba mtu huyo atenda k**a Wao wanavyotenda
✍️Kabla ya mwanadamu kukosea Mungu alikuwa akimtazama mwanadamu anavyoishi,anavyotenda na kuenenda anaiona sura na mfano wake

Kwa hiyo Mungu alipompa mwanadamu uwezo wa kushiriki uumbaji kupitia familia ,alikusudia watu wataokaozalishwa,wawe wanafanana na wanaowazaa na kwa sababu wanaowazaa wanafanana na Mungu na wao wawe na sura na mfano wa Mungu.

Leo mambo yametuwia tofauti kwa sababu sisi kwanza tumepoteza sura na mfano wa Mungu hivyo tunawazaa pia wanapoteza sura na mfano wa Mungu

✍️Maana ya familia kibiblia ni Muunganiko wa mwanamume na mwanamke ambapo unatengeneza watoto/kizazi kwa sura na mfano wao(kinatenda k**a wao,tabia za ndani,mwenendo,tamaduni haiba k**a wao),hivyo wazazi wanapokuwa wanawatazama waliowazaa wanajiona wao

K**a baba na mama ni chemchem ambazo zimetoa mkondo mwingine wa maji hakuna namna maji yale yakawa tofauti na chanzo(labda yakutane na kemikali njiani) ,hivyo watoto hawawezi kuwa tofauti na wazazi labda walikutana na taka katika njia

✍️Kwa njia hizi tunaweza kurejesha tena ile maana ya familia:

Mithali 24:3-4
[3]Nyumba hujengwa kwa hekima,
Na kwa ufahamu huthibitika,

[4]Na kwa maarifa vyumba vyake hujazwa
Vitu vyote vya thamani na vya kupendeza.

Proverbs 24 : 3
Through skillful and godly Wisdom is a house (a life, a home, a family) built, and by understanding it is established [on a sound and good foundation],

Proverbs 24 : 4
And by knowledge shall its chambers [of every area] be filled with all precious and pleasant riches.

Hapa tunaona mambo matatu makubwa

✍️Tutafute maarifa kutoka kwenye chanzo sahihi na cha kweli
✡️Tutafute sababu maarifa hayatatufuata lazima tuingie gharama ya kutafuta

Mithali 4:7
[7]Bora hekima, basi jipatie hekima;
Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.

Mithali 18:15
[15]Moyo wa mwenye busara hupata maarifa;
Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.

Mithali 15:14
[14]Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;
Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.

✡️Maarifa kutoka kwenye chanzo sahihi kilichotuumba na kuumba taasisi hii kongwe kuliko zote duniani,ukitaka taarifa kuhusu simu za iPhone lazima tuende kwa watengenezaji wa iPhone

Mithali 1:7
[7]Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.

✍️Tuyaelewe maarifa na kuweza kuyauhusianisha na maisha yetu

Tutafakari kwa kina na tumuombe Mungu ili tuelewe maarifa tuliyoyatafuta na kuyauhusianisha na maisha yetu

✍️Tuyatumie maarifa tuliyotafuta na kuyaelewa ,hii ndio hekima na ndicho kitakachotuletea tofauti,katika kuyatumia lazima kuomba busara

✡️Busara ni kutambua hekima ipi ya kutumia wapi na kwa wakati gani

Mfano tuna watu wengi leo ambao wanausema upendo lakini hawauelewi ndio maana ,upendo unawavuta kuwa pamoja lakini pindi zinapoonekana dosari, zina waachanisha

Kwa hiyo tunapaswa kuulewa upendo,hekima za upendo,na kuzitumia

Mwisho daima tumwombe Mungu kila siku maarifa,hekima ,uelewa na busara

Tusiishie kuwa na maarifa ambayo hatuyaelewi wala kuyatumia ,maana yatakuwa hayana msaada

Mungu akubariki sana,mshirikishe na mwingine kwa pamoja turejesha misingi ya familia




05/05/2026

Hellow za wakati huu tena
Karibu tuendelee kujifunza na leo kwa neema ya Mungu nataka tupitie kwa ufupi umuhimu wa nafasi aliyotupa Mungu

Kwanza tuitambue ili kuithamini alafu tuanze kuitumia

✍️ Mungu kwa utaratibu aliwejiwekea ni kwamba roho hisiyo na mwili haiwezi kutawala duniani,ndio maana ugomvi mkubwa wa ufalme wa giza na nuru ni umiliki wa mwanadamu ili kumtumia kutawala duniani

Hii ndio maana shetani alivyotaka kumdanganya mwanadamu alitafuta mwili wa kuvaa,lakini majini na mapepo yote huwa wanatafuta miili ya kuvaa ili kuendana na kanuni ya Mungu ya utawala wa hapa duniani

✍️Mungu ameweka utaratibu wa kutokutenda jambo lolote duniani bila mwanadamu.

Sasa tuwaangalie watumishi hawa wawili

✍️Eliya
Mungu alimwambia Eliya akajionyesha kwa Ahabu mvua itanyesha lakini cha kushangaza Eliya alipofanya hivyo Mvua haikunyesha

1 Wafalme 18:1
[1]Ikawa baada ya siku nyingi, neno la BWANA likamjia Eliya, katika mwaka wa tatu, kusema, Enenda, ukajionyeshe kwa Ahabu; nami nitaleta mvua juu ya nchi.

Mungu alisubiri mpaka Eliya aliposimama kwenye nafasi yake akasema neno ,k**a ambavyo alisema kwenye kuizuia mvua ndipo mvua ikanyesha

1 Wafalme 17:1
[1]Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, K**a BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.

1 Wafalme 18:41-42
[41]Naye Eliya akamwambia Ahabu, Haya! Inuka, ule, unywe; kwani pana sauti ya mvua tele.

[42]Basi Ahabu akainuka ili ale na kunywa. Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi, akainama uso mpaka magotini.

✍️Ibrahim
Mungu alikuwa amekusudia tayari kuiharibu sodoma na gomora kulikuwa na ulazima gani wa kumueleza Ibrahim?

Mwanzo 18:17,23,32
[17]BWANA akanena, Je! Nimfiche Ibrahimu jambo nilifanyalo,

[23]Ibrahimu akakaribia, akasema, Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu?

[32]Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema mara hii tu, Huenda wakaonekana huko kumi? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao kumi.

Hapa tunaona Ibrahim akijadiliana na Mungu na alipokomea Ibrahim Mungu akamsikiliza inamaana k**a Ibrahim angeendelea kuomba mpaka mwisho Mungu angeirehemu sodoma na gomora

Nasema hivi kwa sabau ukisoma mistri ifutayo utaona vitu vya ajabu sana

Isaya 41:21,28
[21]Haya, leteni maneno yenu, asema BWANA; toeni hoja zenu zenye nguvu, asema mfalme wa Yakobo.

[28]Na nitazamapo, hapana mtu, hata katika watu hao hapana mshauri mmoja, ambaye, nikimwuliza, aweza kunijibu neno.

Isaya 45:11
[11]BWANA, Mtakatifu wa Israeli, na Muumba wake, asema hivi; Niulize habari za mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari ya kazi ya mikono yangu; haya! Niagizeni.

Isaya 6:8
[8]Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.


Ezekieli 22:30
[30]Nami nikatafuta mtu miongoni mwao, atakayelitengeneza boma, na kusimama mbele zangu mahali palipobomoka, kwa ajili ya nchi, nisije nikaiharibu, lakini sikuona mtu.

✍️Wakati wote Mungu anatafuta mtu aliyesimama kwenye nafasi yake ili ashirikiane naye na kushauriana naye juu ya mambo anayotaka kutenda duniani ,hamna jambo linalotokea kwa kushutukiza .

Uwekezaji wa Mungu duniani ni Passive income 😂

Mungu akubariki sana mshirikishe na mwingine tuendelee kujifunza asante



04/05/2026

Hellow ,Bwana Yesu asifiwe ,za week hii tena

Karibu katika ukurasa huu tuendelea kujifunza pamoja

Na leo nataka tuangalia jambo lifuatalo

✍️Mamlaka ya mtu kutawala dunia na vyote vilivyomo alipewa rohoni kwanza kabla ya mwilini

Mwanzo 1:26-27
[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

[27]Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

✍️Baada ya hii mamlaka sasa ndipo akamleta duniani kimwili sasa ,hivyo kutawala ni kiroho kwanza kabla haijawa kimwili

Mwanzo 2:7
[7]BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

Sasa wajibu wetu mkubwa ni kutambua namna ya kutumia nafsi kuunganisha utawala wa kiroho na wa kimwili utawala wetu uwe halisi

Ufunuo wa Yohana 5:10
[10]ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.

✍️Ndio maana wote wanaotawala kimwili ni wale wenye nguvu kiroho
Husijaribu kutaka kuanzia mwilini kwenda rohoni utakwama au utaishia maisha ya kawaida tuu

Wenye nguvu na wanaojua kwamba wanazo na kutambua namna ya kuzitumia wanatawala ulimwengu

Tujifunze kwa yai likipasuka kutoka nje kwenda ndani ni mwisho wa maisha lakini likipasuka kutokea ndani kuja nje ni mwanzo wa maisha mapya.

Ubarikiwe na Mungu karibu tuendelee kujifunza



30/04/2026

Habari za wakati huu tena mpendwa karibu katika ukurasa huu tuendelee kujifunza

Tuanze kuangalia majibu ya makala iliyopota,na tuanzie hapa

✍️Leo Marekani anapambana na Iran sababu kubwa ni hataki Irani amiliki nyukilia ili Yeye abaki kuwa taifa lenye nguvu na mamlaka.

✍️Leo wengi tunataka kwenda mbinguni (peponi) sababu tumeahidi kwamba tutakuwa na utawala juu ya mazingira(hakuna magonjwa,madeni,umaskini,taabu,manyayaso na masumbufu yote ya duniani)

Kwa hiyo kikubwa wanadamu tunachotafuta ni utawala juu ya mazingira na kimsingi ndicho tulichopoteza ,sababu ndicho ambacho Mungu alitupa

Mwanzo 1:26
[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

✍️Yesu alivyoona wanadamu tunavyoteseka kutafuta vitu ambavyo bado kila kutapopata tunabaki na uhitaji akaamua atuelekeze na kutuonyesha tunachopaswa kutafuta ,na njia ya kukipata

Mathayo 6:33
[33]Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

Sababu tuliumbwa kutawala kwa mfano wa Mungu na uongozi Wake tulipokosea mamalaka hiyo ikaondoka na ndipo masumbuko ya duniani yakaanza.

Kwa hiyo tulichopoteza ni uwepo wa Mungu kwenye maisha yetu,kazi ilibaki ile ile lakni inafanyika bila uwepo wa Mungu pamoja na mfanyaji(mtawala)

Mwanzo 2:15
[15]BWANA Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.

Mwanzo 3:23
[23]kwa hiyo BWANA Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa.

✍️Kwa hiyo tunachopasa kutafuta ni ufalme wa Mungu ,katika huo ndipo kuliko na uwezesho na urejesho wa kutawala tena

Changamoto ni kwamba wengi tunaamini ufalme wa Mungu ni mpaka tuondoke katika maisha haya ndipo tutaenda kuupata lakini imani hii si sahihi sana ,embu soma mistari hii

Mathayo 6:9-10
[9]Basi ninyi salini hivi;
Baba yetu uliye mbinguni,
Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako uje,

[10]Mapenzi yako yatimizwe,
hapa duniani k**a huko mbinguni.

Luka 17:21
[21]wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu.

✍️Kutokana na imani na mtazamo tulionao juu ya ufalme wa Mungu ,umetupelekea kushindwa kutambua ikiwa tumeshaupata au bado hivyo tunashindwa kuutumia.

Nikutie moyo embu anza kujifunza kwa kina kuhusu ufalme wa Mungu,bila kujali dini au dhehebu lako tafuta kuujua na kuuelewa ufalme wa Mungu

Mungu akubariki sana sana

Want your school to be the top-listed School/college in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address

633
Dar Es Salaam
65