Kuna ombwe kubwa kati ya maarifa anayopata mtu na jinsi ya kuyatumia katika kutatua changamoto mbalimbali katika maisha ya kila siku.
Kwa kutumia uzoefu wa miaka 10 katika ujasiriamali tunaamini kwamba tunaweza kuchangia katika kuwapa vijana wa Tanzania fursa ya kujitathimini, kuchukua hatua, na kujenga Tanzania imara kiuchumi. Kijana anayemaliza elimu msingi, elimu ya sekondari, au elimu ya juu anakuwa hana elimu mbadala kumsaidia kutumia kile alichojifunza kutatua changamoto zinazomkabili. Changamoto ya ukosefu wa ajira rasmi
ni tatizo linalokua kila mwaka. Vijana wengi wanaingia mtaani wakiwa hawafahamu wafanye nini kujipatia kipato. FURSA tunaamini kwamba elimu ya ujasiriamali ni moja ya suluhisho nyingi ambazo zinaweza kusaidia kumpa mtu yeyote maarifa na ujuzi wa kutengeneza ajira yake mwenyewe na hata kuajiri watu wengine. Ili kijana atatue changamoto yeyote ni lazima apate maarifa. Maarifa yanapatikana kwa kusoma na kujifunza. FURSA tuna miongozo 8 ambayo inamsaidia kijana kujiandaa kikamilifu kuingia mtaani na kujenga maisha yake mwenyewe – kwa kujiajiri.
1. Jinsi ya kuandaa wazo la biashara
2. Kutengeneza mpango wa Biashara
3. Kugharimu biashara katika ujasiriamali
4. Kutunza kumbukumbu katika biashara
5. Manunuzi na udhibiti wa mali za biashara
6. Mpango mkakati wa kusimamia biashara yako
7. Masoko na Mauzo katika biashara
8. Kusimamia wafanyakazi katika biashara yako
Kwa kutumia uzoefu wa miaka 10 katika ujasiriamali tunaamini kwamba tunaweza kuchangia katika kuwapa vijana wa Tanzania fursa ya kujitathimini, kuchukua hatua, na kujenga Tanzania imara kiuchumi.