Mwl Eng Goodluck Mushi

Mwl Eng Goodluck Mushi

Share

+255764402453

28/05/2026

Hallelujah
Kijana mwenzangu naomba tupambane pamoja hatuna Muda k**a tunavyofikiri
Tujitahidi KUUKOMBOA WAKATI maana ZAMANI HIZI NI ZA UOVU.

WAEFESO 5:15-17
KUMBUKA:
Ukifika mahali unapotakiwa kuwepo kwa Ibada au kazi au kikao n.k kabla ya Muda UMEWAHI, na Ukifika Kwa WAKATI ni umechelewa maana kuna mambo utashindwa kuyaweka sawa maana Muda umeshafika na KUCHELEWA haikubaliki.
MUNGU AKUBARIKI SANA

19/05/2026

Bwana Yesu asifiwe
Hallelujah
Kwenye Maisha wapo watu huja na Tochi kwenye maisha yako katikati ya Giza Nene. Usaiwasahau kamwe wala Kuwadharau. Ni kweli kuna wanaoweza kuwa na madhaifu fulani na ukaona k**a mwisho haukuwa mzuri saana kwasababu ya Tabia na Haiba fulani lakini hili Halikupi Ruhusa ya Kumdharau wewe Muombee kwa Bwana maana bado ana Umuhimu mkubwa kwenye Historia ya Maisha yako.
MUNGU AKUBARIKI SANA

01/05/2026

Bwana Yesu asifiwe,
Msaada Mkubwa wa Mungu kwa Mtu ni KULITUMA NENO LAKE.
Omba sana Mungu akupe KUSIKIA,KUTAMBUA,KUELEWA,KUKUBALI NA KUTII hilo Neno.
Maana ndani ya NENO kuna KESHO YAKO.
Isaya 55:10-11

Mungu akubariki sana

11/04/2026

Bwana Yesu asifiwe,
Katika MAJIRA tuliyo nayo Moja ya Jambo la Kutilia Maanani ni *KUSHIKA SANA ULICHONACHO*. Kila kitu Mungu amekupa Ona ni Muujiza na Kipe Umuhimu wake katika Maisha yako Usikitumie Vibaya. Unavyoonesha Uthamani katika Kile Mungu amekupa iwe ni KAZI,BIASHARA, KIPAWA,HUDUMA,FEDHA MKONONI MWAKO n.k unampa Mungu sababu ya Kukibarikia zaidi na Kukulinda bila kujali mazingira na Majira yamekaa kwa namna gani.
Mungu akubariki sana.

By
Mwl Eng Goodluck Mushi

31/03/2026

Shalom mtu wa Mungu
Kati ya eneo tunahitaji saana KUWEKEZA ni kwenye MAARIFA
Hosea 4:6 anazungumza KUANGAMIZWA kwa Kukosa MAARIFA na Warumi 10:2 anazungumza *Kuwa na juhudi katika Mungu lakini si katika MAARIFA"
Hivyo MAARIFA ni ya Muhimu sana sana.
TAFUTA KUJAA MAARIFA ILI KUWA WA KIWANGO MUNGU ANATAKA.
UBARIKIWE SAANA

Heri ya Mwezi wa nne 2026

15/03/2026

Bwana Yesu asifiwe,
Mtu Kufika Mahali alipofika kuna Gharama yake kubwa saana. Usidharau kamwe mahali mtu amefika. Ile kwamba Haukuwa naye wakati anaua Dubu na Simba machungani usimdharau anapokwambia anaenda Kumpiga Goliati maana imengharimu SIRINI kuandaliwa na Kujiandaa.
Neema ya Mungu ituwezeshe kuheshimu gharama ya mtu aliyoingia kufika Mahali alipofika.
Ubarikiwe saana

12/03/2026

Yakobo 5:16
"Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, *akiomba kwa bidii*.

Mungu akubariki sana

10/03/2026

Zaburi 124
8 Msaada wetu u katika jina la Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.

Mungu akubariki sana

23/02/2026

BWANA YESU ASIFIWE.
Vijana wenzangu tuishi HUKU. ISHI uhalisia hapana kuishi maisha yasiyo halisi. Maisha yasiyo halisi ni ghali saana. (Fake Life is Very Expensive). MUNGU AKUBARIKI SANA

12/02/2026

Hallelujah
Mungu ni Mwaminifu humwinua mtu Hatua kwa Hatua. Pale Mungu amekupa Neema ya Kuanzia usipadharau anza Pamoja naye na Uombe Uso wa Bwana uende pamoja nawe. Hakikisha unafurahia Kila hatua na kumwamini Mungu anayekuchakata.
MAISHA NI MCHAKATO.
UBARIKIWE SAANA

Want your school to be the top-listed School/college in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Website

Address

P. O Box
Dar Es Salaam