Hallelujah
Kijana mwenzangu naomba tupambane pamoja hatuna Muda k**a tunavyofikiri
Tujitahidi KUUKOMBOA WAKATI maana ZAMANI HIZI NI ZA UOVU.
WAEFESO 5:15-17
KUMBUKA:
Ukifika mahali unapotakiwa kuwepo kwa Ibada au kazi au kikao n.k kabla ya Muda UMEWAHI, na Ukifika Kwa WAKATI ni umechelewa maana kuna mambo utashindwa kuyaweka sawa maana Muda umeshafika na KUCHELEWA haikubaliki.
MUNGU AKUBARIKI SANA
Mwl Eng Goodluck Mushi
+255764402453
19/05/2026
Bwana Yesu asifiwe
Hallelujah
Kwenye Maisha wapo watu huja na Tochi kwenye maisha yako katikati ya Giza Nene. Usaiwasahau kamwe wala Kuwadharau. Ni kweli kuna wanaoweza kuwa na madhaifu fulani na ukaona k**a mwisho haukuwa mzuri saana kwasababu ya Tabia na Haiba fulani lakini hili Halikupi Ruhusa ya Kumdharau wewe Muombee kwa Bwana maana bado ana Umuhimu mkubwa kwenye Historia ya Maisha yako.
MUNGU AKUBARIKI SANA
Bwana Yesu asifiwe,
Msaada Mkubwa wa Mungu kwa Mtu ni KULITUMA NENO LAKE.
Omba sana Mungu akupe KUSIKIA,KUTAMBUA,KUELEWA,KUKUBALI NA KUTII hilo Neno.
Maana ndani ya NENO kuna KESHO YAKO.
Isaya 55:10-11
Mungu akubariki sana
Bwana Yesu asifiwe,
Katika MAJIRA tuliyo nayo Moja ya Jambo la Kutilia Maanani ni *KUSHIKA SANA ULICHONACHO*. Kila kitu Mungu amekupa Ona ni Muujiza na Kipe Umuhimu wake katika Maisha yako Usikitumie Vibaya. Unavyoonesha Uthamani katika Kile Mungu amekupa iwe ni KAZI,BIASHARA, KIPAWA,HUDUMA,FEDHA MKONONI MWAKO n.k unampa Mungu sababu ya Kukibarikia zaidi na Kukulinda bila kujali mazingira na Majira yamekaa kwa namna gani.
Mungu akubariki sana.
By
Mwl Eng Goodluck Mushi
Shalom mtu wa Mungu
Kati ya eneo tunahitaji saana KUWEKEZA ni kwenye MAARIFA
Hosea 4:6 anazungumza KUANGAMIZWA kwa Kukosa MAARIFA na Warumi 10:2 anazungumza *Kuwa na juhudi katika Mungu lakini si katika MAARIFA"
Hivyo MAARIFA ni ya Muhimu sana sana.
TAFUTA KUJAA MAARIFA ILI KUWA WA KIWANGO MUNGU ANATAKA.
UBARIKIWE SAANA
Heri ya Mwezi wa nne 2026
15/03/2026
Bwana Yesu asifiwe,
Mtu Kufika Mahali alipofika kuna Gharama yake kubwa saana. Usidharau kamwe mahali mtu amefika. Ile kwamba Haukuwa naye wakati anaua Dubu na Simba machungani usimdharau anapokwambia anaenda Kumpiga Goliati maana imengharimu SIRINI kuandaliwa na Kujiandaa.
Neema ya Mungu ituwezeshe kuheshimu gharama ya mtu aliyoingia kufika Mahali alipofika.
Ubarikiwe saana
Yakobo 5:16
"Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, *akiomba kwa bidii*.
Mungu akubariki sana
Zaburi 124
8 Msaada wetu u katika jina la Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.
Mungu akubariki sana
BWANA YESU ASIFIWE.
Vijana wenzangu tuishi HUKU. ISHI uhalisia hapana kuishi maisha yasiyo halisi. Maisha yasiyo halisi ni ghali saana. (Fake Life is Very Expensive). MUNGU AKUBARIKI SANA
12/02/2026
Hallelujah
Mungu ni Mwaminifu humwinua mtu Hatua kwa Hatua. Pale Mungu amekupa Neema ya Kuanzia usipadharau anza Pamoja naye na Uombe Uso wa Bwana uende pamoja nawe. Hakikisha unafurahia Kila hatua na kumwamini Mungu anayekuchakata.
MAISHA NI MCHAKATO.
UBARIKIWE SAANA
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Category
Contact the school
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam