Ni nani shia?
Download kitabu hapa
http://elmiyah.com/index.php/component/k2/item/172-ushia
Irshaad
Elimu sahihi kwa matazamo wa Qur'ani na Sunnah.
16/07/2015
❄ SIKU YA EID INAPOSADIFU IJUMAA ❄
Zimekuja Hadith kadhaa sahihi toka kwa bwana Mtume صلي الله عليه وسلم na Athar toka kwa Swahaba wa Mtume, kuhusu Siku ya Eid kiangukia Ijumaa. Na baadhi ya Hukumu muhimu k**a ifuatavyo:
1. Imepokewa na Imaam Ahmad, Abuu Dawud, An-Nasaai, Ibnu Maajah, Ad-Daarimy na Al-Haakim: kutoka kwa Zayd bin Arqam رضي الله عنه kwamba MU'AWIYAH BIN ABIY SUFIYAAN رضي الله عنه alimuuliza:
"Je, uliwahi kushuhudia -pamoja na Mtume صلي الله عليه وسلم- Eid mbili zilokutana ndani ya siku moja? Akajibu: Ndio. Akasema (Mu'awiyah) Mtume alifanyaje? Akajibu: Album swali Eid kisha akatoa Rukhsa ya kutosali Ijumaa, akasema hivi: Atakaye kuswali Ijumaa na Aswali.
2. Imepokewa na Al-Haakim, Abuu Dawud, Ibnu Maajah, Ibnu Al-Jaaruudy na Al-Bayhaqy kutoka kwa Abiy Hurayrah رضي الله عنه amesema ya kwamba: Mtume صلي الله عليه وسلم alisema:
"Hakika siku yenu ya leo zimekutana Eid mbili (Eid na Ijumaa) basi anayetaka Swalat ya Eid itakuwa imemtosheleza na Ijumaa (hatolazimika kuswali Ijumaa) ama sisi Tutaswali Ijumaa"
3. Imepokewa na Ibnu Maajah na Twabarany kutoka kwa Ibn Omar رضي الله عنهما amesema:
"Zilikutana Eid mbili zama za Mtume صلي الله عليه وسلم akawasalisha Watu (Eid) kisha akasema: Anayetaka Kuja kuswali Ijumaa na aje, na Anayetaka kurejea NYUMBANI na arejee"
4. Imepikewa na Ibnu Maajah kutoka kwa Ibn Abbas رضي الله عنهما amesema kwamba: Mtume صلي الله عليه وسلم alisema:
"Zimekutana Eid mbili ktk siku yenu ya Leo, basi atakaye (Eid) iatakuwa imemtosheleza kutokana na Ijumaa, ama sisi tutaswali Ijumaa in shaa Allah"
5. Imepokewa na Abuu Dawud na Ibnu Khuzaymah kutaka kwa A'twaa bin Abiy Rabaah amesema: Tulisalishwa na (Abdullah) Ibn Zubeir, Swalat ya Eid asubuhi ktk siku ya Ijumaa. Kisha (baadaye) tukaja (Msikitini) ili Kuswali Ijumaa, hakujitokeza kuja kuswalisha. Basi tukaswali pekee yetu. Wakati huo Ibn Abbas alikuwa TWAAIF, tulipokuja Twaaif tukamsimulia kisa hiki. Akasema "Alipatia Sunnah"
✴ BAADHI YA HUKMU MUHIMU ✴
① Atakayehudhuria Swalat ya Eid basi anaruhusiwa kutoswali Ijumaa na badala yake ataswali Adhuhuri. Ila k**a ataamuwa kuswali na Ijumaa itakuwa bora zaidi
② Yule ambaye hakuhudhuria Swalat ya Eid basi hana Rukhsa ya kuacha Ijumaa siku hiyo. Ila k**a hatopata pahala inaposwaliwa Ijumaa siku hiyo basi ataswali Adhuhuri
③ Inampasa Imaam wa Msikiti Kuisimamisha Swalat ya Ijumaa siku hiyo, ili wataotaka kuhudhuria wahudhurie na pia wale ambao hawakuswali Eid yapate Ijumaa
④ Ikiwa Hakutoswaliwa Ijumaa basi si Rukhsa kuadhini siku hiyo kwa ajili ya Adhuhuri, labda k**a itakuwa ni adhana ya Ijumaa
⑤ Si Kweli kwamba anayeswali Eid siku hiyo basi Haswali Ijumaa na Adhuhuri. Bali ukweli ni kwamba Adhuhuri inamuwajibikia
Allah ataqabali Funga na Dua zetu. Allahumma ameen
http://www.elmiyah.com/index.php/component/k2/item/177-iddi-na-ijumaa
Iddi na Ijumaa kukutana <div class="_5pbx userContent" data-ft="{"tn":"K"}"> <div id="id_55a76cd2b630a3c...
09/04/2015
Assalaam alaykum kwa ambaye anataka kuwekwa katika wasapp ya Manhaji elmiyah
.......Tuma namba yako hapa pamoja na jina
0712450136
Jinsi ya kujilinda na EBORA.............soma ufahamu ndugu
http://www.elmiyah.com/index.php/component/k2/item/169-ebola
03/04/2015
Huu si uislamu je unautambua ...................soma ujionee
http://www.elmiyah.com/index.php/component/k2/item/172-ushia
Huu si uislamu... <p> </p> <p style="text-align: center;"> </p> <p style="text-align: center;"> </p> <p style...
Assalaam alykum
katika tovuti yetu ya Manhaji elmiyah njia ya wajawema waliotangulia imeweka kipengele cha kuweza kusikiliza na kushusha "download" darsa na Qur'ani za matwalibu elmu wenye kutegemewa hapa nchini
http://elmiyah.com/index.php/qur-ani-na-darsa/darsa/abuu-mussa/145-laamiya
15/11/2014
MAANA YA KUFANYA MAKABURI KUWA NI MISIKITI
Kusujudu juu ya kaburi, kwa kulifanya kaburi kuwa ni sehemu ya kusujudia, na anakuwa maiti ndiye mwenye kusujudiwa “Allah atulinde” na hii ni shirki ya waziwazi.
Kuswali kwa kulielekea kaburi, yaani: kaburi kuwa mbele yake halafu akawa anaswali kwa kulielekea na kulifanya kuwa ndio kibla chake, na muabudiwa wake, “Allah atulinde” na hukmu yake ni k**a aina iliyotangulia
Kuswali hali ya kulielekea kaburi; kwa kuitakidi kwamba kuswali pembeni ya kaburi kuna ubora na fadhila nyingi, hata k**a anaswali kwa ajili ya Allah si kwa kuliabudia kaburi, na hii vilevile ni haramu; kwa sababu ni njia ya kuelekea kwenye ile hali ya kwanza na ya pili.
Ni zaidi ya aina zilizopita, nayo ni kuzikwa maiti kwenye ardhi iliyo salama “haina kaburi”, kisha ukajengwa msikiti kwenye ardhi hiyo, au kuwekwa kaburi ndani ya msikiti uliojengwa kwenye ardhi iliyo salama “ambayo haina kaburi”, aina zote mbili ni sawa, na kusudio ni moja, nalo ni kuweka kaburi ndani ya msikiti, na hukmu yake nia sawa na ilyotangulia, na ikiwa kaburi hilo linaabudiwa hiyo ni shirki kubwa yenye kumtoa mtu katika dini ya kiislamu, na ikiwa makusudio ni kuitakidi kwamba kuswali pembeni ya kaburi kuna fadhila zaidi basi itakuwa ni katika madhambi makubwa k**a utavyokuja ubainifu wake.
Kujengwa msikiti pembeni ya kaburi, au kuwekwa kaburi pembeni ya msikiti, hukmu yake ni sawa na iliyotangulia.
Na aina mbaya kabisa ni ile ya mwanzo na ya pili; kwa sababu inamtoa mtu katika uislamu, ama aina zilizobaki ni haramu , hazimtoi mtu katika uislamu, na unakuja ubainifu wake kwa upana katika kipengele vinavyofuata
http://elmiyah.com/index.php/component/k2/item/171-makaburi
15/11/2014
Je? inafaa kuswali katika makaburi...........
http://elmiyah.com/index.php/component/k2/item/171-makaburi
Makaburi misikitini <p class="MsoNormal" style="text-align: center;" align="center"><strong><span style="font-size: 15.0...
13/11/2014
Je? unafahamu maradhi haya......Allah atunusuru na maradhi haya
http://elmiyah.com/index.php/component/k2/item/169-ebola
Ugonjwa wa Ebola <p style="text-align: center;"><strong>MARADHI YA EBOLA</strong></p> <p><strong>Ebola</strong> ni...
13/11/2014
Assalaam alaykum,alhamdullilah tumeanza kuifanikisha tovuti yetu baada ya kutokuwa hewani kwa muda mfupi..........
Tunakuomba tupe mawazao juu ya tovuti hii mpya.....
http://elmiyah.com/index.php
05/09/2014
Manhaji Elmiyah - Ugonjwa wa ebola Ebola ni ugonjwa wa hatari unaosababishwa na virusi vijulikanavyo kwa lugha ya kitaalamu “Ebola Virus”. ugonjwa wa damu kutoganda. Ugonjwa huu ni mion...
Irshaad Elimu sahihi kwa matazamo wa Qur'ani na Sunnah.
Click here to claim your Sponsored Listing.