Irshaad

Irshaad

Share

Elimu sahihi kwa matazamo wa Qur'ani na Sunnah.

Iddi na Ijumaa kukutana 16/07/2015

❄ SIKU YA EID INAPOSADIFU IJUMAA ❄

Zimekuja Hadith kadhaa sahihi toka kwa bwana Mtume صلي الله عليه وسلم na Athar toka kwa Swahaba wa Mtume, kuhusu Siku ya Eid kiangukia Ijumaa. Na baadhi ya Hukumu muhimu k**a ifuatavyo:

1. Imepokewa na Imaam Ahmad, Abuu Dawud, An-Nasaai, Ibnu Maajah, Ad-Daarimy na Al-Haakim: kutoka kwa Zayd bin Arqam رضي الله عنه kwamba MU'AWIYAH BIN ABIY SUFIYAAN رضي الله عنه alimuuliza:

"Je, uliwahi kushuhudia -pamoja na Mtume صلي الله عليه وسلم- Eid mbili zilokutana ndani ya siku moja? Akajibu: Ndio. Akasema (Mu'awiyah) Mtume alifanyaje? Akajibu: Album swali Eid kisha akatoa Rukhsa ya kutosali Ijumaa, akasema hivi: Atakaye kuswali Ijumaa na Aswali.

2. Imepokewa na Al-Haakim, Abuu Dawud, Ibnu Maajah, Ibnu Al-Jaaruudy na Al-Bayhaqy kutoka kwa Abiy Hurayrah رضي الله عنه amesema ya kwamba: Mtume صلي الله عليه وسلم alisema:

"Hakika siku yenu ya leo zimekutana Eid mbili (Eid na Ijumaa) basi anayetaka Swalat ya Eid itakuwa imemtosheleza na Ijumaa (hatolazimika kuswali Ijumaa) ama sisi Tutaswali Ijumaa"

3. Imepokewa na Ibnu Maajah na Twabarany kutoka kwa Ibn Omar رضي الله عنهما amesema:

"Zilikutana Eid mbili zama za Mtume صلي الله عليه وسلم akawasalisha Watu (Eid) kisha akasema: Anayetaka Kuja kuswali Ijumaa na aje, na Anayetaka kurejea NYUMBANI na arejee"

4. Imepikewa na Ibnu Maajah kutoka kwa Ibn Abbas رضي الله عنهما amesema kwamba: Mtume صلي الله عليه وسلم alisema:

"Zimekutana Eid mbili ktk siku yenu ya Leo, basi atakaye (Eid) iatakuwa imemtosheleza kutokana na Ijumaa, ama sisi tutaswali Ijumaa in shaa Allah"

5. Imepokewa na Abuu Dawud na Ibnu Khuzaymah kutaka kwa A'twaa bin Abiy Rabaah amesema: Tulisalishwa na (Abdullah) Ibn Zubeir, Swalat ya Eid asubuhi ktk siku ya Ijumaa. Kisha (baadaye) tukaja (Msikitini) ili Kuswali Ijumaa, hakujitokeza kuja kuswalisha. Basi tukaswali pekee yetu. Wakati huo Ibn Abbas alikuwa TWAAIF, tulipokuja Twaaif tukamsimulia kisa hiki. Akasema "Alipatia Sunnah"

✴ BAADHI YA HUKMU MUHIMU ✴

① Atakayehudhuria Swalat ya Eid basi anaruhusiwa kutoswali Ijumaa na badala yake ataswali Adhuhuri. Ila k**a ataamuwa kuswali na Ijumaa itakuwa bora zaidi

② Yule ambaye hakuhudhuria Swalat ya Eid basi hana Rukhsa ya kuacha Ijumaa siku hiyo. Ila k**a hatopata pahala inaposwaliwa Ijumaa siku hiyo basi ataswali Adhuhuri

③ Inampasa Imaam wa Msikiti Kuisimamisha Swalat ya Ijumaa siku hiyo, ili wataotaka kuhudhuria wahudhurie na pia wale ambao hawakuswali Eid yapate Ijumaa

④ Ikiwa Hakutoswaliwa Ijumaa basi si Rukhsa kuadhini siku hiyo kwa ajili ya Adhuhuri, labda k**a itakuwa ni adhana ya Ijumaa

⑤ Si Kweli kwamba anayeswali Eid siku hiyo basi Haswali Ijumaa na Adhuhuri. Bali ukweli ni kwamba Adhuhuri inamuwajibikia

Allah ataqabali Funga na Dua zetu. Allahumma ameen

http://www.elmiyah.com/index.php/component/k2/item/177-iddi-na-ijumaa

Iddi na Ijumaa kukutana <div class="_5pbx userContent" data-ft="{&quot;tn&quot;:&quot;K&quot;}"> <div id="id_55a76cd2b630a3c...

Photos from Irshaad's post 09/04/2015

Assalaam alaykum kwa ambaye anataka kuwekwa katika wasapp ya Manhaji elmiyah
.......Tuma namba yako hapa pamoja na jina
0712450136

Photos 15/11/2014

MAANA YA KUFANYA MAKABURI KUWA NI MISIKITI

Kusujudu juu ya kaburi, kwa kulifanya kaburi kuwa ni sehemu ya kusujudia, na anakuwa maiti ndiye mwenye kusujudiwa “Allah atulinde” na hii ni shirki ya waziwazi.

Kuswali kwa kulielekea kaburi, yaani: kaburi kuwa mbele yake halafu akawa anaswali kwa kulielekea na kulifanya kuwa ndio kibla chake, na muabudiwa wake, “Allah atulinde” na hukmu yake ni k**a aina iliyotangulia
Kuswali hali ya kulielekea kaburi; kwa kuitakidi kwamba kuswali pembeni ya kaburi kuna ubora na fadhila nyingi, hata k**a anaswali kwa ajili ya Allah si kwa kuliabudia kaburi, na hii vilevile ni haramu; kwa sababu ni njia ya kuelekea kwenye ile hali ya kwanza na ya pili.

Ni zaidi ya aina zilizopita, nayo ni kuzikwa maiti kwenye ardhi iliyo salama “haina kaburi”, kisha ukajengwa msikiti kwenye ardhi hiyo, au kuwekwa kaburi ndani ya msikiti uliojengwa kwenye ardhi iliyo salama “ambayo haina kaburi”, aina zote mbili ni sawa, na kusudio ni moja, nalo ni kuweka kaburi ndani ya msikiti, na hukmu yake nia sawa na ilyotangulia, na ikiwa kaburi hilo linaabudiwa hiyo ni shirki kubwa yenye kumtoa mtu katika dini ya kiislamu, na ikiwa makusudio ni kuitakidi kwamba kuswali pembeni ya kaburi kuna fadhila zaidi basi itakuwa ni katika madhambi makubwa k**a utavyokuja ubainifu wake.
Kujengwa msikiti pembeni ya kaburi, au kuwekwa kaburi pembeni ya msikiti, hukmu yake ni sawa na iliyotangulia.

Na aina mbaya kabisa ni ile ya mwanzo na ya pili; kwa sababu inamtoa mtu katika uislamu, ama aina zilizobaki ni haramu , hazimtoi mtu katika uislamu, na unakuja ubainifu wake kwa upana katika kipengele vinavyofuata
http://elmiyah.com/index.php/component/k2/item/171-makaburi

Maskani 13/11/2014

Assalaam alaykum,alhamdullilah tumeanza kuifanikisha tovuti yetu baada ya kutokuwa hewani kwa muda mfupi..........
Tunakuomba tupe mawazao juu ya tovuti hii mpya.....
http://elmiyah.com/index.php

Maskani

Manhaji Elmiyah - Ugonjwa wa ebola 05/09/2014

Manhaji Elmiyah - Ugonjwa wa ebola Ebola ni ugonjwa wa hatari unaosababishwa na virusi vijulikanavyo kwa lugha ya kitaalamu “Ebola Virus”. ugonjwa wa damu kutoganda. Ugonjwa huu ni mion...

05/09/2014

Irshaad Elimu sahihi kwa matazamo wa Qur'ani na Sunnah.

Want your school to be the top-listed School/college in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Address

Dar Es Salaam