HIVYO ULIVYO LEO NI MATOKEO YA UNAVYOFIKIRI
MAANA VILE MTU AJIONAVYO NAFSINI MWAKE NDIVYO ALIVYO
MITHALI 23:7
Mafanikio & Biashara Yako
Learning about Business and Entrepreneur
HIVYO ULIVYO LEO NI MATOKEO YA UNAVYOFIKIRI
MAANA VILE MTU AJIONAVYO NAFSINI MWAKE NDIVYO ALIVYO
MITHALI 23:7
27/04/2025
Hizi hapa njia 7 za haraka kabisa za kuwa masikini
1.Tumia Pesa Zako Zote Bila Kuweka Akiba
Kwa nini uweke akiba wakati maisha ni leo? Tumia hadi senti ya mwisho… halafu kopa tena!
2.Epuka Kujifunza Mambo Mapya
Kitabu ni mzigo, semina ni utapeli, kozi ya mtandaoni ni kupoteza muda. Elimu ni kwa watoto wa shule tu!
3.Kwepa Fursa Zote Mpya
“Biashara ni ngumu”, “Hii inaonekana ni scam”, “Sina muda”… zungumza hivyo kila mara unapoona nafasi mpya ya maendeleo.
4.Tegemea Mshahara Pekee Maisha Yote
Kazi moja tu kwa miaka yote. Usiwaze kuhusu kipato cha pili. Malipo ya mshahara yanatosha hata k**a hutoshi.
5.Lalamika Kila Siku, Kaa Bila Hatua
Lalamikia serikali, bei ya bidhaa, familia yako, au majirani… lakini usithubutu kuchukua hatua yoyote ya kubadilika.
6.Shindana Badala ya Kujifunza kwa Waliokutangulia
Ukiwaona waliokuzidi, anza kuwalaumu au kuwaonea wivu. Usione kwamba unaweza kujifunza kitu kwao.
7.Tumia Kila Siku Kusaka Starehe Tu
Muda wote Facebook, TikTok, Netflix… usingizi mwingi, outing kila weekend. Maisha ni kufurahia tu mengine kesho.
Sasa k**a HUTAKI kuwa masikini, epuka hizi tabia.Anza kujifunza, tafuta fursa, tengeneza vyanzo vya kipato, na jifunze kila siku.Maisha bora ni matokeo ya maamuzi bora!
Usipobadilika sasa hakuna namna maisha yako yatakwenda kubadilika.
Upo tayari kubadilika?
Wapi unahitaji support?
Karibu https://wa.link/tam8ul
21/04/2025
Tunza Dhamira
Dhamira ni hali kuwa na shauku Imara ya kupata kitu au hali.
Shauku hiyo itazaa ubunifu. Penye Nia Pana njia zinazokubalika.
Nia huonekana kupitia utayari na kuendelea kufanya yanayotakiwa hata k**a Kuna ugumu.
Bidii inapokufa, hofu na visingizio huingia.
18/04/2025
Celebrating my 7th year on Facebook. Thank you for your continuing support. I could never have made it without you. 🙏🤗🎉
Usije ukakata tamaa....
Mara nyingi nguvu unayoiweka kwenye kuliendea jambo lako huwa ni kubwa lakini matokeo huja kwa uchache sana.
*SIRI*
Ili ufanikiwe unatakiwa uhesabu zaidi mafanikio uliyoyapata na yakupe nguvu ya kurudia kufanya tena na tena na tana na tena napo ndiyo tunakamilisha ule usemi wetu wa haba na haba.....
Mvumilivu hula......
*Happy Good Friday*🙏🙏
18/04/2025
Unafahamu utofauti kati ya elimu na taaluma?
Ukichanganya hapa utajichanganya kwenye maisha yako.
Kuna tofauti kati ya kufundishwa na kujifunza.
Jifunze kujifunza ili usilaumu system na wazazi uweze kuishi maisha yakwako na uwe mwinyesha njia kwenye maisha ya wengine.
Karibu tusaidiane 0676029497
22/09/2024
Uchaguzi wako ndiyo Maisha yako
Mungu hakupi kitu usichokitaka
Unalo chaguo la kumtumikia Mungu au Shetani.
Ukimtumikia Shetani utafanikiwa ila hutabarikiwa na ukimtumikia Mungu utafanikiwa na utabarikiwa....
Njia ya shetani ni rahisi lakini ni Ngumu badae wakati ya Mungu ni Ngumu sana mwanzoni na inakatisha tamaa lakini mwishowe huwa rahisi na yakudumu.
Mafanikio halisi yamefichwa chini kabisa ya matatizo na hutayapata mpaka uamue kuzitafuna changamoto zote mpaka ziishe.
Shortcut may be a long cut and Long Cut may be a Shortcut
Chaguo ni lako uila usifanye kwaajili ya wengine kuwa mkubwa simama mwenyewe, anza upya (Reborn) kila kitu kinawezekana mbele ya Mungu ukiamua tu.
20/09/2024
Mafanikio yamefichwa chini kabisa ya msoto.
10/06/2024
MKULE CHURA WAKONKWANZA
Chura ni mambo ya msingi tunayotakiwa kuyafanya.
Tusisahau kufanya majukumu yetu Yale ya msingi kwanza mapema bila kujali tunajisikiaje Kwa Wakati huo maana mambo ya maana yanachosha na kunyong'onyesha sana mwanzoni.
Basi usisogeze mbele Kwa kujiambia utafanya badae ukipata muda.
Jipe hata dakika 2 tu kila Siku mapema za kuyafanya utashangaa umeongeza muda na hatimaye umetoboa.
Uwe na Siku nzuri na wiki yenye ufanisi na mafanikio makubwa sana ukakutane na matarajio yako makubwa uliyoyasubiri Kwa muda mrefu sana🙏🙏
12/05/2024
KARIBU SANA KESHO ASUBUHI KUANZIA SAA 1:00 ADUBUHI HADI SAA 3:00 ASUBUH TUTAKUWA LIVE KWENYE CHANEL YA KUZUNGUMZIA KWA UNDANI UELEWA WA JAMII KUHUSU MAGONJWA YANAYOSABABISHWA NA ULAJI USIOFAA.
USIKOSE NA SHIRIKISHA WENGINE NAAMINI WENGI SANA WATABARIKIWA SANA KWA KIPINDI HIKI MAANA TUNAMWENDA KUGUSA KWENYE KWENYE MSHONO KABISA.
TUOMBEANE HERI ILI KESHO TUAMKE SALAMA NA TUKAJUMUIKE.
SEE YOU....🙏🙏
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Category
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam