Balewa Daycare Centre

Balewa Daycare Centre

Share

NI SHULE YA AWALI NA MSINGI INAYOPOKEA WANAFUNZI WENYE UMRI KUANZIA MIAKA MIWILI NA NUSU. MTAALA WA KUFUNDISHIA NI KIINGEREZA.

18/08/2025

NI BUUUURREE....!!! WAHI SASA!!

10/11/2022

Wapendwa wazazi, walezi na wadau wa elimu,
kwa unyenyekevu mkubwa kabisa tunapenda kuwaalika katika Siku ya Wazazi itakayofanyika shuleni siku ya Jumamosi tarehe 26/11/2022 kuanzia saa tatu kamili asubuhi mpaka saa nane kamili mchana. Karibu ujionee wanachokipata watoto wakiwa shuleni. Karibu ujionee kazi yetu. Tutafurahi sana kuwa nawe.

Mkurugenzi

21/11/2021

Wapendwa wazazi, walezi na wadau wa elimu,
Kwa unyenyekevu mkubwa kabisa tunapenda kuwaalika katika Siku ya Wazazi itakayofanyika shuleni siku ya Jumamosi tarehe 27/11/2021 kuanzia saa tatu kamili asubuhi mpaka saa sita kamili mchana. Karibu ujionee wanachokipata watoto wakiwa shuleni. Karibu ujionee kazi yetu. Tutafurahi sana kuwa nawe.

Mkurugenzi

27/10/2021

KARIBU UCHUKUE FOMU YA KUJIUNGA NA MASOMO MWAKA 2022 LEO.

08/09/2021

Tunawatakia kila la heri wahitimu wote wa Darasa la Saba wanaoanza mitihani yao ya Taifa leo. Mwenyezi Mungu awatangulie na kuwaepusha na kila shari. Ameen

Mkurugenzi

07/04/2021

CHETI CHA USAJILI WA BALEWA DAYCARE

17/03/2021

TANZIA
Uongozi wa Balewa Daycare Centre umepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John Joseph Pombe Magufuli kilichotokea tarehe 17-3-2021. Tunatoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote. Tunaungana na Watanzania wenzetu katika maombolezo ya msiba huu mkubwa kwa taifa letu. Mwenyezi Mungu atujaalie subira na badala ya tulichopoteza.
Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea.

Mkurugenzi

23/02/2021

BALEWA NURSERY AND PRIMARY SCHOOL INAELEWA HALI NGUMU YA UCHUMI TUNAYOPITIA NA NDIO MAANA:

-ADA ZETU NI NAFUU SANA.
-ADA ZETU TUNATOZA KWA MWEZI.
-MZAZI HALIPII MIEZI AMBAYO MTOTO HAJASOMA.

SAMBAMBA NA HILO, TUNAZINGATIA UBORA WA HUDUMA ZOTE WAPATAZO WATOTO WANAPOKUWA SHULENI.

NAFASI ZINAPATIKANA KWA MADARASA YA AWALI NA DARASA LA I-III.
SHULE INAPATIKANA DAR ES SALAAM, KIBAMBA MONGONI. KM 2 NA NUSU KUTOKA KIBAMBA NJIAPANDA YA SHULE.

JIUNGE NASI LEO.
TUPIGIE: +255712964348

Balewa Daycare Centre Send a message to learn more

02/02/2021

SHUKRANI
Kwa niaba ya uongozi wa Balewa Daycare Centre na Balewa Nursery and Primary School, napenda kutoa shukrani za dhati kabisa kwa wazazi, walezi na wadau wote wa elimu waliotuamini na kutuunga mkono. Hakika mmeonesha imani kubwa sana kwetu. Nasi jukumu letu ni kuhakikisha kuwa hatuwaangushi. Tunamwomba Mwenyezi Mungu tuwe sehemu ya ujenzi wa kizazi bora kabisa kitaaluma na kimaadili. Tunamwomba pia Mwenyezi Mungu atujaalie sote uwezo wa kutimiza majukumu yetu kikamilifu kwa ustawi wa watoto wetu. Kwa pamoja tunaweza.
Asanteni sana.
Mkurugenzi

04/01/2021

HUJACHELEWA BADO!!

31/12/2020

Mkurugenzi wa Balewa Daycare Centre kwa heshima kubwa kabisa anapenda kutoa shukrani za dhati kwa wafanyakazi wote, wazazi, walezi, wanafunzi na wadau wote wa elimu kwa ushirikiano mkubwa mliouonesha mwaka huu 2020 katika kutimiza malengo ya taasisi yetu. Hakika mafanikio yote tuliyofikia ni kutokana na ushirikiano mliotupa. Mmekuwa chachu ya huduma bora na ya viwango. Tunawaomba muendeleze ushirikiano huu zaidi katika mwaka ujao wa 2021. Tunawatakia kila la heri katika mwaka 2021. Mwenyezi Mungu awabariki sana! Asanteni sana!
Mkurugenzi

Want your school to be the top-listed School/college in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Website

Address


Kibamba_Mongoni
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 15:00
Tuesday 08:00 - 15:00
Wednesday 08:00 - 15:00
Thursday 08:00 - 15:00
Friday 08:00 - 15:00