14/01/2026
Uongozi wa serikali ya wanafunzi DARUSO -SoED kutoka chuo kikuu Cha Dar es salaam Leo Jan 14 2026 wamefanikiwa kufanya mazungumzo na uongozi wa kampuni ya SWIFPACK inayojishughulisha na usafirishaji ndani ya shirika la Posta Tanzania ...
.
Mazungumzo hayo yalilenga kujenga ushirikiano wa kufanya KAZI pamoja na Namna Bora ya kufanikisha Bonanza la Wanafunzi wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2025/2026 katika ofisi ya Posta Makao makuu.
Bonanza hilo linatarajiwa kufanyika siku ya Tarehe 31 Jan 2026 kwa kuwashirikisha wanafunzi wote wa Shule kuu ya Elimu (SoED) pamoja na kawaalika wanafunzi Kutoka college of Humanities (COHU) na wale wanafunzi wa DUCE .....
Hivyo mpaka sasa majadiliano yapo pazuri kuhakikisha mambo yanakaa vizuri Ili kuanza matangazo ya haraka... .tanzania
11/01/2026
Viongozi wa Shule kuu ya Elimu DARUSO -SoED M/kiti Danford Millanzi na Katibu wake Vedastus Gunda ni miongoni mwa viongozi wa Muhimili wa Mahalliama katika serikali ya wanafunzi chuo kikuu Cha Dar es salaam DARUSO Mlimani waliohudhuria kikao KAZI Cha Muhimili huo Jan 9 2026 ndani ya viunga vya Chuo Kikuu Cha Dar es salaam Kampasi ya Mwalimu Nyerere (Main campus).....
11/01/2026
Tujiandae kwa tarehe tajwa
02/01/2026
Uongozi wa serikali ya wanafunzi Kutoka Shule kuu ya Elimu DARUSO -SoED unakupongeza sana Prof. Rose Upor kwa kuteuliwa kuwa Makamu mkuu wa chuo Taaluma (DVC - ACADEMIC) .....
28/12/2025
Huu ndio muonekano Hali wa majengo ya Chuo Kikuu Cha Dar es salaam Kampasi ya Lindi iliyowekwa jiwe la Msingi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dr. Mwigulu Lameck Nchemba na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na taasisi mbalimbali...
.
Udsm yazidi kung'ara ...
28/12/2025
Mguu wa roho mguu wa shingo hakuna kutetereka mtaelewa tu , safi kabisa ..
Unapoenda kazini hakikisha jembe unalo begani k**a mchezaji na mpira na viatu ....
Maandalizi hayo kuelekea Intercollege 2026...
28/12/2025
Mimi kwangu Hawa ni wakombozi kwenye SOKA la UDSM unaweza kuchukulia poa lakini wanapokuwa kwenye majukumu yao k**a vile siyo wale wanaoingia Darasani ....
Muite Hugo Master bonge la Full back hakuna kupita kirahisi ....
.
Tunawakaribisha wote mkaribie mtakaposikia Intercollege imeanza njoo uone vipaji ...
Ahsante sana vijana wangu kutoka Shule kuu ya Elimu SoED ...
28/12/2025
Nyumbani kwanza ambapo ni SOED...
Nawaamini sana wanangu mnapokuwa kazini hakuna kurudi nyuma mwanzo mwisho ...
Mpaka tone la mwisho , Mmeniahidi makubwa nasisi k**a uongozi tunawaahidi ushirikiano mkubwa Ili mambo yawe makubwa zaidi....
Vijana wa mpira wa migumu kutoka Shule kuu ya Elimu chuo kikuu Cha Dar es salaam UDSM ...
HAKUNA KUPOA...
28/12/2025
Kesho la Maangamizi la Shule kuu ya Elimu DARUSO -SoED Wana jambo Lao mwaka huu ..
Hakuna kupoa mpaka kieleweke wanangu ....
Mwaka Jana wanajua kilicho wakuta wengine kwahiyo kila Kona kwa sasa maelezo ni SoED footballer team....