24/12/2022
CAREER DEVELOPMENT
Kipi bora kujiajiri au kuajiriwa? Usifanye haraka kujibu swali hili. Fikiri kwa kina kwanza.
Kila upande utakao chagua una faida na hasara. Itategemea wewe unatafuta nini katika maisha yako.
Natambua unalo jibu lako.Hebu tuangalie faida za kila kimoja. Baada ya hapo utakuwa katika nafasi nzuri ya kuweza kuchagua upande unaoutaka.
FAIDA ZA KUAJIRIWA
1️⃣Uhakika wa kipato kila baada ya muda fulani. Kipato chako kinatabirika hivyo ni uhakika.
2️⃣Unakuwa katika nafasi nzuri kuweza kukopesheka na taasisi za fedha. Taasisi za fedha ziko tayari kumkopesha mtu mwenye kipato cha kuaminika (reliable source of income)
3️⃣Kujihakikishia kiinua mgongo au pensheni ya uzeeni.
4️⃣Fursa ya bima ya afya kwa wafanyakazi huwa ni rahisi zaidi.
5️⃣Ni shughuli ambayo haina risk kubwa. Hakuna uwezekano wa kupoteza pesa zako. Upande wa kujiajiri kuna wakati unapoteza mtaji wako kutokana na kupata hasara.
6️⃣Mbali na mshahara unaweza kupata marupumarupu ya hapa na pale pamoja na safari za kulipiwa.
FAIDA ZA KUJIAJIRI
1️⃣Mtu aliyejiajiri anapata faida za kodi (Tax advantages).Mwajiriwa hawezi kuepuka makato ya kodi kirahisi.
2️⃣Uhuru wa muda wako. Una maamuzi na muda wako. Unaamua kuutumia upendavyo wewe.
3️⃣Uhuru mkubwa zaidi wa maamuzi. Unakuwa na uhuru wa kufanya maamuzi yako bila kuingiliwa au kupangiwa na mtu mwingine.
4️⃣Uwezekano wa urithishaji. Mradi au shughuli binafsi unaweza kurithisha kwa watoto au ndugu zako. Lakini ajira hakuna kurithisha.
5️⃣ Uwezekano wa kuingiza mapato makubwa zaidi. Kwa aliyejiajiri hakuna ukomo wa kipato chake k**a ilivyo kwa mwajiriwa. Kadiri biashara inavyokwenda vizuri na kipato hupanda zaidi na zaidi.
6️⃣Kuna uwezekano wa kutajirika kwa haraka sababu biashara haitabiriki k**a ilivyo kwa ajiri. Mazingira yakiwa mazuri unatoka haraka.
Vp, bado una msimamo wako ule ule juu ya masuala haya? Nimeeleza upande wa faida pekee. Sijaeleza hasara au madhaifu ya kila upande.
Wewe unayo nafasi ya kuchagua unataka kuwa nani. Si jambo zuri kufuata mkumbo. Angalia malengo yako ni nini hasa. Kisha chagua upande unao utaka. Mimi si wale wanaoshinda wanadanganya watu mitandaoni.
Shea na marafiki
_____________
The best way to learn is to learn from the best
24/12/2022
Kuna pahala ifike tuache kujidanganya
wenyewe. Kuna pahala ifike Visingizio uamue kuviweka pembeni na kupambania kweli kile umedhamilia.
K**a unasema unakosa usingizi
sababu ya Maono uko nayo, Basi kweli
uwe unakosa usingizi sababu ya watu wengine wengi tu ambao wanawezakuwa tegemeo Lao 📌
23/04/2022
K**a wewe ni kijana, mjasiriamali ama muajiriwa na ungependa kuongeza mkondo wa kipato kupitia mda wako wa ziada bila kuathiri shughuli zako za sasa wasiliana na si kwa namba +255716712618 au bonyeza link
👇👇
https://wa.me/255716712618 kuja moja kwa moja WhatsApp kwa muongozo zaidi.
03/03/2022
MASWALI 7 YA KUJIULIZA KABLA HUJALALA, KUHUSU HALI YAKO YA KIFEDHA
1.Je leo umeandika kila pesa uliyopata kwa uaminifu bila kupuuzia wala kudharau kiwango chake?
2.Je leo umeandika kila pesa iliyotoka mkononi mwako (uliyotumia) kwa uaminifu bila kujidanganya wala kupuuzia udogo au ukubwa wa pesa husika?
3.Je, unajua jumla ya mapato yako na Jumla ya matumizi yako kwa leo tu?
Uwiano wake upoje?
Balance yako ipoje? Ni hasi au chanya?
5.Je leo umejitahidi kupunguza gharama za matumizi kadiri ilivyowezekana?
6.Kuna kitu chochote umenunua ambacho ulikuwa hujapanga kukinunua?
7.Je leo katika pesa uliyoipata umeweka akiba?
K**a ndiyo! Hongera.
K**a hujaweka akiba, kwanini?
Tafakari malengo yako ya mwaka, jipime mwenendo wako, halafu jijibu k**a ukiendelea hivyo, UTAFIKA?
k**a jibu ni hapana. jiulize itakuwaje...
03/03/2022
Adui Wa Malengo Yako Ni Tabia Ya Kughairisha Malengo...
Unashindwa kutimiza malengo yako kwa sababu ya kusema utafanya baadae au kesho na sio kuchukua hatua ya kuanza...
..sasa ili uweze kutimiza malengo yako
Una malengo makubwa sana ya;
1. Biashara, unapenda kuwa mfanyabiashara kubwa na mwenye kufanikiwa kwenye eneo la biashara
2. Ujasiriamali, kuna fursa umeiona na umeweka malengo kuwa fursa hiyo itabadili kabisa Maisha yako
3. Huduma, malengo kuwa Huduma yako itakuwa kubwa sana na mwenye mwenye ushawishi kupitia Huduma yako
4. Mahusiano, una malengo mahusiano yako kudumu kwa muda mrefu kwa kuwajibika ipasavyo kwenye mahusiano yako
5. Kipaji, Una malengo kuwa kipaji chako ukiendeleze kitakuingizia kipato na kuwa ajira yako
Nakadhalika
Una malengo makubwa sana lakini unashindwa kupiga hatua kwenye maisha yako sababu
Unasema utafanya kesho na kesho ikifika unasema utafanya kesho nyengine kiasi kesho nyingi pasipo kufanya
Unasema utafanya mwakani na mwakani ikifika unasema utafanya mwaka unaokuja pasipo kufanya
Unasema utafanya baadae na baadae ikifika unasema utafanya baade tena pasipo kufanya
Kwa maana hiyo!
Ili utimize malengo yako ni lazima ushinde tabia ya kughairisha malengo yako
Kushinda tabia ya kughairisha ni pamoja na kuanza kufanya muda huo huo yani sasa
Usisubiri uwe na kila kitu ndio uanze Hakuna “Parfect Time” ya kuanza zaidi ya wewe kuanza na kile ambacho unacho
Kushinda tabia ya kughairisha Tumia Kanuni ya dakika mbili (Two Minutes Rule)
Kazi yeyote ambayo unaweza kufanya chini ya dakika mbili ifanye mara moja bila kusubiri
Ukifanya kazi kwa dakika mbili utaweza kufanya zaidi ya dakika mbili na hii mbinu inaitwa kutrick ubongo wako kutoka kwenye eneo la kuridhika “Comforting Zone” na kuendelea kufanya kazi husika
Acha kughairisha malengo yako sasa kwa kutumia Kanuni ya dakika mbili
Je wewe unafanya nini ili kushinda tabia ya kughairisha malengo yako?
Kauli Mbiu: “Maisha Ni Kuthubutu”
______
ZINGATIA: “Muda sahihi wa kutimiza malengo yako ni sasa na sio kesho”
_______