28/05/2026
TAARIFA MUHIMU KWA WAHITIMU NA WAZAZI
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limetangaza rasmi kufunguliwa kwa dirisha la udahili kwa ngazi ya Astashahada (Certificate) na Stashahada (Diploma) kwa mwaka wa masomo 2026/2027 kuanzia leo, tarehe 28 Mei, 2026.
14/05/2026
🎓 FAHAMU MFUMO WA POINTI ZA NECTA! 📚
Je, unajua pointi zako zinaamua daraja lako la ufaulu?
Hapa tumekuandalia mwongozo rahisi wa kuelewa madaraja ya Kidato cha Nne (CSEE) na Kidato cha Sita (ACSEE) kulingana na mfumo wa NECTA. ✅
📌 Kwa wanafunzi:
Tambua ulipo na ujipange kufika juu zaidi! 💪
📌 Kwa wazazi:
Msaidie mwanao kuelewa namna ufaulu unavyopimwa na umuhimu wa kuongeza juhudi kwenye masomo.
🏆 Kumbuka:
“Pointi chache = ufaulu mkubwa zaidi.”
🔥 Endelea kutufuatilia kwa taarifa sahihi za elimu, ushauri wa masomo na mbinu za kufaulu mitihani.
02/05/2026
Safari ya miaka miwili ya jitihada, kulala usiku kucha na kusoma kwa bidii sasa inakwenda kuzaa matunda.
Tunawatakia kila la heri wanafunzi wote wa Kidato cha Sita (Form VI) kote nchini, na hasa mashujaa wetu wa Moonlight Open Secondary School, mnapoanza mitihani yenu ya Taifa (ACSEE) tarehe 4 May 2026.
26/04/2026
🎉 Heri ya Sikukuu ya Muungano!
Kutoka Moonlight Academy – tunalea kizazi chenye maadili, maarifa na uzalendo.
🇹🇿 26 April 2026
21/04/2026
Je, ulishawahi kukutana na changamoto ya majina kukosewa kwenye cheti chako? 🤔
NECTA wanakumbushea kuwa jukumu la kuhakiki usahihi wa majina ni lako wakati wa usajili. Baada ya hapo, hakuna marekebisho ya kuongeza jina yatakayofanyika.
Share taarifa hii na mdogo wako au mwanafunzi aliye karibu nawe asije akapoteza fursa muhimu huko mbeleni. 📌
04/04/2026
Heri ya Pasaka kutoka Moonlight Open Secondary School! 🕊️✨
Tunapoadhimisha ufufuo na matumaini mapya, uongozi wa shule unawatakia wanafunzi wetu, wazazi, na wadau wote heri ya sikukuu ya Pasaka. K**a ilivyo kauli mbiu yetu—"Excellence in Student's Achievement"—tunaamini kuwa kila msimu mpya unakuja na fursa mpya za kung'ara kimasomo na kimaadili.
Mapumziko mema na yenye baraka tele kwa familia zenu! 🐣📚