17/10/2022
Mzalendo Kizimbani
Sehemu ya 15
Sekondari alisoma mbali na nyumbani. Shule ya serikali iliyokuwa mkoa wa mbali na ilikuwa ya bweni. Mara moja Baba alipata taarifa kuwa Mako kaonekana mjini, akapiga simu shule, akaambiwa kijana yupo na anasoma kwa bidii.
Baada ya kumaliza kidato cha nne, kidato cha tano na sita hakikuchukua muda, alimaliza na kwenda kulitumikia jeshi la kujenga taifa kwa miezi mitatu. Baadae alianza chuo kikuu akisomea shahada ya elimu. Mara tano Baba alienda chuo kumtafuta ili amjulie hali, hakumkuta, lakini alipewa taarifa mwanafunzi huyo yupo ila huonekana muda wa vipindi na haishi katika eneo la chuo. Baba alipomuuliza Mako, akajibu anaishi eneo la chuo na huonekana hapo muda wote. Hata hivyo akasisitiza Baba anapotaka kuja kumtembelea atoe taarifa kwani hujificha sehemu kujisomea na kufanya iwe ngumu kuonekana na watu wengine.
Alimaliza chuo, akakaa nyumbani wiki moja halafu akasema amepata shule kufundisha. Jina la shule alilotaja Baba alilitafuta hakulipata. Mako alishakuwa mtu mzima, alimuacha na maisha yake.
Mako aliondoka nyumbani akisema anafundisha katika shule yake isiyofikika. Muda mwingi hakuonana na Baba lakini waliwasiliana. Hata hivyo, huwezi kumpata Mako mpaka yeye akupigie. Ili kuwatoa hofu wazazi, Mako aliwapigia mara moja kila mwezi, akawaambia anaendelea vizuri na mambo yananyooka wasihofu!
Katika jiji kuu la Nchi Yetu, katika uwanja wa Uhuru watu wengi walifurika wakiwemo viongozi wa mataifa mbalimbali. Wote walifika kushuhudia tukio la kuapishwa kwa rais mpya wa Nchi Yetu, Mzee Mnyonge!
Baba alikuwa miongoni mwa watu waliokataa kupitwa na shughuli hii ya kihistoria. Alikaa uwanjani siti ya mbele akilitazama jukwaa alilopaswa kukaa Rais mpya, Mzee Mnyonge. Hata hivyo leo alionekana kuwa makini na asiyeamini alichokiona mbele yake. Alikaa katika mshangao ule kwa saa kadhaa mpaka Mzee Mnyonge alipoapishwa.
Sasa Mzee Mnyonge baada ya kuwa rais mpya, akakaa katika kigoda. Alivaa suruali ya mtumba nyeusi, shati jeupe lililovaliwa mara kadhaa na tai nyekundu ambayo inaonekana alilazimishwa kuivaa ili kuzingatia itifaki. Mkono wa kulia alishika mkuki, kushoto alik**ata ngao iliyochorwa rangi za bendera ya Nchi Yetu. Baba aliendelea kumtazama mtu aliyemtazama kwa muda mrefu. Mtu huyo alisimama nyuma ya rais Mzee Mnyonge. Alivalia kofia ya askari, Koti jekundu lililotiwa nakshi za kijeshi k**a kamba na mikufu iliyotambaa maeneo ya juu. Kijana huyu alikuwa mpambe wa rais, kwa jina la kimombo akiitwa ‘aide-de-camp’ lakini huko mtaani, watu humuita ‘bodigadi’ japo hiyo si kazi yake. Baba alimshangaa sana kijana huyo. Si kwamba alishangaa kijana wa umri mdogo kupewa jukumu hilo kubwa, au alishangaa mavazi aliyovalia la! Baba alimfahamu kijana huyo, alikuwa Mako!
Kuwa wa kwanza kupokea mwendelezo wa riwaya hii kwa kujiunga katika group hili... https://chat.whatsapp.com/EJMKHncJobzH2IhhPVSvCC
22/09/2022
14/09/2022
06/09/2022
03/09/2022
01/09/2022
23/08/2022
19/08/2022
18/08/2022
17/08/2022
16/08/2022