05/04/2026
تابعوا مسابقة القرآن الكريم العالمية 2026، المقامة في ملعب بنيامين ويليام مكابا، دار السلام – تنزانيا، بتاريخ 05/04/2026
ضيف الشرف الرسمي:
رئيس زنجبار الدكتور حسين علي مويني.
الضيف الخاص:
إمام المسجد الحرام – مكة المكرمة، المملكة العربية السعودية.
شاهدوا البث المباشر عبر الرابط:
اضغط هنا للمشاهدة المباشرة
https://www.youtube.com/live/OWLY2gBnKO0?si=BhoEWUrerHDnq9dl
لا تنسوا:
المشاركة، والاشتراك، والتعليق.
AL AMEEN TV 📺
🔴 #LIVE MASHINDANO YA DUNIA YA QUR'AN TUKUFU BENJAMIN MKAPA STADIUM 05/04/2026
Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.
21/03/2026
Angalia Baraza la EID KUPITIA AL AMEE N TV
🔴 #LIVE BARAZA LA EID EL FITRI KITAIFA DAR ES SALAAM
Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.
14/03/2026
Zakatul-Fitr ni zaka inayotolewa mwishoni mwa mwezi wa Ramadhan kabla ya Swala ya Eid al-Fitr.
1. Lengo la Zakatul-Fitri
Hikma yake
Mtume ﷺ amesema:
عن ابن عباس رضي الله عنهما قال:
فرض رسول الله ﷺ زكاة الفطر طُهرةً للصائم من اللغو والرفث وطُعمةً للمساكين.
رواه أبو داود.
Maana yake:
Mtume ﷺ ameifaradhisha Zakatul-Fitri ili:
Kumsafisha aliyefunga kutokana na makosa madogo aliyoyafanya wakati wa kufunga.
Kuwasaidia maskini ili nao wapate chakula siku ya Idi.
2. Kiwango cha kutoa
Mtume ﷺ amesema:
فرض رسول الله ﷺ زكاة الفطر صاعًا من تمر أو صاعًا من شعير...
رواه البخاري ومسلم
Maana:
Mtume ﷺ amefaradhisha Zakatul-Fitri Saa moja (صاع) ya chakula.
Kiwango chake
1 Saa = takribani kilo 2.5 – 3 za chakula.
Chakula kinachotolewa hutegemea chakula kikuu cha watu wa eneo husika.
Mfano:
Mchele
Ngano
Mahindi
Tende
3. Ni nani anatakiwa kutoa
Zakatul-Fitri
Ni wajibu kwa
Kila Muislamu
Mwenye chakula cha ziada siku ya Idi
Hutolewa kwa ajili ya:
Nafsi yake
Watoto wake
Watu anaowalea
4. Muda wa kutoa
Wakati wa kutoa una ngazi tatu:
1. Wakati bora
Baada ya kuzama jua mwisho wa Mwezi Mtukufu Ramadhan mpaka kabla ya Swala ya Idi
2. Inaruhusiwa mapema
Siku 1 au 2 kabla ya Idi
K**a ilivyofanywa na Maswahaba.
3. Ikiwa atatoa baada ya Swala ya Idi
Mtume ﷺ amesema:
من أداها قبل الصلاة فهي زكاة مقبولة ومن أداها بعد الصلاة فهي صدقة من الصدقات
رواه أبو داود
Maana: Mwenye kutoa
Kabla ya Swala ya Idi itakuwa Zaka sahihi na Mwenye kutoa
Baada ya Swala inakuwa sadaka tu
5. Je inafaa kutoa pesa badala ya chakula?
Wanazuoni wamekhitalifiana:
Rai ya wengi
(Jamhuri ya wanazuoni)
K**a:
Imam Malik
Imam al-Shafi'i
Imam Ahmad ibn Hanbal
Wanasema:
➡️ Inatolewa chakula si pesa kwa sababu hiyo ndiyo aliyofanya Mtume ﷺ.
Rai ya baadhi ya wanazuoni
K**a:
Imam Abu Hanifa
Wanasema:
➡️ Inaruhusiwa kutoa pesa ikiwa ni manufaa zaidi kwa maskini.
Taasisi ya AL AMEEN FOUNDATION - AIF inakusanya na KUGAWA na ZAKKATUL FITRI kwa makundi Maalum.
WASILISHA Zakatul Fitri Yako Kupitia Namba za Simu
+255 715 800 772
+255 657 277 747
Matarajio siku ya KUGAWA ni Siku Moja Kabla ya EID
08/02/2026
Asalaam alaikum
Kuelekea Mwezi Mtukufu wa Ramadhani TAASISI YA AL AMEEN FOUNDATION AIF .
Inapenda kukushirikisha wewe Mpenda kheiri katika kuchangia PROGRAM HII MAALUM ya Iftar Kwa Makundi Maalum katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Matarajio kugawa iftar Awamu ya kwanza kabla Mwezi wa Ramadhani.
Vifaa ambavyo Tunavyo hitaji kukusanya
1.Mchele
2.Tambi
3.Unga Ngano
4.Maharage
5.Sukari
6.Mafuta
7.Tende n.k
Tuikimbilie kheiri hii.
Mawasiliano zaidi : 0715800772
11/01/2026
Watoto wetu wanufaika wa PROGRAM YA ORPHANS BACK TO SCHOOL 2026 inayo simamiwa na Taasisi ya AL Ameen foundation - AIF wakiongoza Dua ya Shukran kwa wadau walio changia Program hii kabla ya Zoezi la Ugawaji .
Tukio zima unaweza lishuhudia kupitia Youtube chanel yetu : AL AMEEN TV
au Bonyenza Link hii : https://www.youtube.com/live/xgnXmAukK8A?si=5O-_fLs1JqcHXOb6
10/01/2026
Alhamdulillāh 🤲
Kwa fadhila na rehema za Mwenyezi Mungu ﷻ, jambo limepita salama katika program ya Orphans Back to School 2026 iliyoandaliwa na Taasisi ya Al Ameen Foundation – AIF.
Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuwafikia watoto yatima 150 na kuwapatia msaada unaowasaidia kurejea shule wakiwa na matumaini mapya.
Taasisi ya Al Ameen Foundation – AIF inatoa shukrani za dhati kwa wafadhili wote, wadau, viongozi, wanachama na kila aliyeshiriki kwa hali na mali katika kufanikisha mradi huu wa kheri.
Mwenyezi Mungu awabariki, awaongezee riziki, na ayakubali matendo yenu mema.
Program hii ni ushahidi kwamba ushirikiano katika kheri huleta matokeo makubwa, na kwa pamoja tunaendelea kujenga kesho bora kwa watoto yatima kupitia elimu na malezi mema.
📚🤝 Orphans Back to School 2026
Chini ya uratibu wa Taasisi ya Al Ameen Foundation – AIF
🟢 Kauli mbiu:
“Kusema na Kutenda Ndiyo Msingi wa Maendeleo kwa Jamii.”
Mwenyezi Mungu atujalie tuendelee kuwa sababu ya kheri kwa wengine. Aamiin.
10/01/2026
Alhamdulillāh 🤲
Kwa uwezo na neema za Mwenyezi Mungu , leo tarehe 10/01/2026, Taasisi ya AL AMEEN FOUNDATION – AIF imefanikiwa kugawa vifaa vya shule kwa watoto yatima wapatao 150, ikiwa ni sehemu ya juhudi zetu za kuinua elimu, utu na matumaini ya watoto wetu.
Hafla hii tukufu ilipambwa na uwepo wa viongozi na wanazuoni mbalimbali wa dini, wakiongozwa na:
Sheikh Mohammed Nassor Amran – Kiongozi Mkuu wa Taasisi
Sheikh Omar Mgaza – Kutoka Ofisi ya M***i
Sheikh Dau Silima – Kutoka Waqf na Mali Amana Zanzibar (Kitengo cha Zakaah na Sadaka)
Sheikh Ahmad Rajab Msomi – Kutoka Chuo Kikuu cha Al Azhar Shareef, Misri.
Viongozi hawa walitoa nasaha, dua na hamasa, wakisisitiza umuhimu wa kuwalea yatima kwa misingi ya dini, elimu na maadili mema, sambamba na kushirikiana katika kazi za kheri kwa ajili ya radhi za Mwenyezi Mungu.
Tunatoa shukrani za dhati kwa wafadhili wote, wadau, wanachama na kila aliyeshiriki kwa njia moja au nyingine kufanikisha tukio hili.
Mwenyezi Mungu awalipe kheri nyingi, abariki mali zenu na aweke matendo haya katika mizani ya mema.
📌 AL AMEEN FOUNDATION – AIF itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhudumia jamii, kusaidia yatima na kuwekeza katika elimu kwa ajili ya kizazi cha leo na kesho.
“Na wanakuuliza watumie nini. Sema: Kheri mnayotoa ni kwa wazazi, jamaa, yatima, masikini na wasafiri.” (Al-Baqarah: 215)
🤝 Karibu tushirikiane katika kheri.
Goreeb & Yateem Trust Fund
Kijana Wa Kiislam Dsm
Kijana wa Kiislam Tanzania
Najivunia kuwa Bint wa Kiislam
Najivunia kuwa Muislam
10/01/2026
Zoezi la Ugawaji wa Vifaa vya Shule kwa watoto Yatima 2026 , *AL AMEEN FOUNDATION -AIF*
LINAFANYIKA KIJITONYAMA ALIMAUA
🔴LIVE # ZOEZI LA UGAWAJI VIFAA VYA SHULE NA DUA KWA WATOTO YATIMA 2026
Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.
07/01/2026
ASalaam alaikum
Karibuni saana
Kwa wale wanao taka kuchangia
0797 800 772
0657 277 747
AL AMEEN FOUNDATION AIF