06/12/2022
Prof. Issa Shivji na Jenerali Ulimwengu leo walikuwa SJMC kuendesha mhadhara wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) kuhusu Azimio la Dar es Salaam juu ya Uhuru wa Uhariri na Uwajibikaji (DEFIR)
Akifungua mhadhara huo Dkt. Mona amewataka washiriki wakiwemo wanafunzi wa shule hiyo kutumia fursa hiyo ya kipekee kujifunza na kuifanyia kazi elimu watakayoipokea.
04/12/2022
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinafanya utafiti fuatilizi (tracer study) ili kifanye upitiaji wa programu zinazotolewa katika vitengo vyake mbalimbali.
Dr. Mona Mwakalinga, Dean na Dr. Gidion Kamfipo tunakuomba ujaze e-dodoso letu k**a wewe ni mhitimu wetu wa B.A, na M.A (Journalism, PRA na Masscommunication) ili tupate maoni yako kuhusiana na programu tunazotoa.
Maoni yako ni muhimu sana. Tunakuhakikishia kwamba taarifa zako zitakuwa kwa ajili ya zoezi husika tu.
Maoni yako yatatusaidia wakati wa kupitia programu zetu zetu.
Zoezi la kujaza *e-dodoso* litachukua muda kidogo ila tunaomba ujitahidi mpaka ufike mwisho na umetuma.
NB: Uanzapo kujaza page ya kwanza ukishachagua SJMC bonyeza "view SJMC survey" na usibonyeze kwenye Next iliyopo page hiyo ya kwanza.
Kwa changamoto Mpigie Fanuel Hume - 0782549992
Karibu ujaze e-dodoso kwa kufuata *kiunzi (link)* hapo chini.
*Asante sana kwa ushirikiano wako.*
https://edodoso.gov.go.tz/index.php/828257
02/12/2022
JAMII FORUMS YAENDESHA MDAHALO NA WANAFUNZI WA SJMC KUHUSU USHIRIKI WA VIJANA KATIKA MICHAKATO YA KIDEMOKRASIA NCHINI
Uongozi wa Asasi ya kiraia inayohusika na uchechemuzi katika haki za kidigitali,kiraia,kidemokrasia,utawala bora na uwajibikaji (JAMII FORUMS) imeendesha na inatarajia kuendelea muendeshamijadala endelevu na fikra mbadala kwa vyuo takribani 8 ndani ya kipindi cha miezi 6 katika kutatua changamoto mbalimbali za vijana kwenye jamii.
Akizungumza Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Forums Maxence Melo wakati akiwa katika shule kuu ya uandishi wa habari ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam ambapo Jamii Forums iliandaa mdahalo wa vijana uliohusu nafasi na ushiriki wa vijana katika michakato ya kidemokrasia nchini amesema wamelenga kuandaa mijadala endelevu na fikra mbadala vyuoni ili kuwafanya vijana wawe na uvumilivu hususani kwenye siasa na uwezo wa kufikiri zaidi katika utatuzi wa changamoto za jamii
Aidha Max amesema Uongozi wa Jamii Forums umefarijika kutoa elimu ya kutosha kwa vijana chuoni hapo kuhusiana na demokrasia na kuongeza kuwa ushiriki wa vijana katika mdahalo huo umekuwa mpana zaidi kutokana na elimu waliyoipata katika mdahalo huo.
Grace Mdoe mwanafunzi wa mwaka wa 3 katika shule kuu ya uandishi wa habari amesema kupitia warsha hiyo chuoni hapo wamepata fursa ya kuzungumza na kuwaondoa woga wa kupaza sauti zao kwenye jamii
Vilevile wanafunzi hao wamekiri kuwa kupitia ujio wa jamii forums chuoni hapo wamejifunza vyema namna ya kuwasilisha mawazo yao mbele za watu katika hafla mbalimbali
JAMII FORUMS YAENDESHA MDAHALO NA WANAFUNZI WA SJMC KUHUSU USHIRIKI WA VIJANA KATIKA MICHAKATO YA KIDEMOKRASIA
Uongozi wa Jamii umeendesha na unatarajia kuendelea kuendesha mijadala endelevu kwa vijana katika vyuo takribani 8 ndani ya kipindi cha miezi 6 katika kutatua changamoto mbalimbali za vijana kwenye jamii.
Akizungumza katika mdahalo huo, Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Forums Maxence Melo amesema Jamii Forums imelenga kuandaa mijadala endelevu na fikra mbadala vyuoni ili kuwafanya vijana wawe na uvumilivu hususani kwenye siasa na uwezo wa kufikiri zaidi katika utatuzi wa changamoto za jamii
Aidha, Max amesema kuwa uongozi wa Jamii Forums umefarijika kutoa elimu kwa vijana kwa vijana chuoni hapo kuhusiana na demokrasia na kuongeza kuwa ushiriki wa vijana katika mdahalo huo umekuwa mpana zaidi kutokana na elimu waliyoipata katika mdahalo huo.
Kwa upande wao wanawanafunzi wa SJMC wamekiri kuwa kupitia ujio wa Jamii Forums chuoni hapo wamejifunza vyema namna ya kuwasilisha mawazo yao mbele za watu katika hafla mbalimbali
30/11/2022
Dr. Judith Wanda na Dr. Victor Eliah wamehitimu shahada za Uzamivu katika Fani ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma
30/11/2022
Hongera Dk. Issa Mbura kutunukiwa PhD leo kwenye mahafali ya 52.
29/06/2022
#60 years UDSM anniversary🔥