16/06/2022
Mathayo 24:4-14
[4]Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye.
[5]Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.
[6]Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.
[7]Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.
[8]Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu.
[9]Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.
[10]Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana.
[11]Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi.
[12]Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.
[13]Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
[14]Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.
29/04/2022
12/11/2021
22/01/2021
21/06/2019
11/06/2019